KOCHA WA AZAM FC AFUNGIWA MECHI TATU NA KUPIGWA FAINI YA LAKI 5


Kocha wa Azam FC, Aristica Cioaba amefungiwa mechi tatu na kupigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa kuwafuata waamuzi na kuwalalamikia kwa kurusha mikono akionyesha kutoridhika na maamuzi yao.

Alifanya hivyo kwenye mechi namba 69 ya Ligi Kuu ya Vodacom dhidi ya Ruvu Shooting iliyofanyika Novemba 4, 2017 kwenye Uwanja wa Azam ambapo azam Fc walishinda wa bao 1-0 .




Na adhabu hiyo kali imezingatia Kanuni ya 40(1) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Makocha. Ambapo makocha wote wanahitajika kutokukiuka kwa kanuni hiyo muhimu

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527