HAYA NDIYO MAAMUZI MENGINE YA RAIS MAGUFULI,BANDARI ZOTE KULINDWA NA JESHI LA POLISI




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amelitaka jeshi la polisi nchini kurejesha kitengo cha ulinzi bandarini na pia eneo ambalo linafungwa mita za mafuta.


Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, imesema Rais Magufuli ametaka jeshi la polisi nchini kurejesha ulinzi kama ilivyokuwa nyakati za nyuma kabla mamlaka ya bandari haijaamua kubandilisha mfumo wa kuweka walinzi wake.


Balozi Ombeni Sefue ameongeza kuwa katika eneo ambalo linafungwa mita za mafuta (Flowmeters), ambalo waziri mkuu alitembelea na kumsimamisha mkurugenzi wa wakala wa vipimo sasa ni lazima lilindwe na jeshi la polisi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527